MWANASHERIA
Emmanuel Muga amelionya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuotiita timu
ya taifa, Kilimanjaro Stars, kwani kufanya hivyo ni kinyume cha mkataba
wa udhamini wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL).
Muga
alikuwa Mwanasheria wa TFF wakati inasaini mkataba wa udhamini na SBL
kwa ajili ya timu ya taifa Mei 12, mwaka huu katika hoteli ya Serena
mjini Dar es Salaam.
Na
leo Muga amesema; “Mimi ndiye niliyeshughulikia na kusaini mkataba wa
kuidhamini timu ya taifa. Sharti moja kuu ni kwamba, timu isiitwe tena
Kilimanjaro Stars. Wanaona kama ni kuendelea kuwapa thamani Kilimanjaro
(Bia), wadhamini wa zamani. Msikiuke mkataba, msiite Taifa Stars Kili
Stars, hata iweje,”.
Mei
12, SBL iliingia mkataba wa udhamini wa Sh. Bilioni 2.1 kwa miaka
mitatu na TFF juu ya Taifa Stars katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi
wa Kivukoni 4, hoteli ya Serena, Dar es Salaam, hiyo ikiwa mara ya pili
kwao, baada ya awali kuidhamini timu hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu
kuanzia 2008 hadi 2011.
Katika
mkataba huo, SBL iliwakilishwa na Mkurugenzi wae Mkuu, Mholanzi Mama
Helene Weesie na TFF iliwakilishwa na Rais wake wa wakati huo, Jamal
Malinzi.
Juhudi
za haraka za john ndeki Online kumpata Katibu Mkuu wa TFF,
Wilfred Kidau kulizungumzia hilo hazikufanikiwa na hata Msemaji, Alfred
Lucas hakupatikana pia.
Lakini
inafahamika Taifa Stars ni timu ya taifa ya muungano inayohusisha na
wachezaji wa Zanzibar pia, wakati timu ya Bara imekuwa ikijulikana kwa
jina la Kilimanjaro Stars na Zanzibar kuna Zanzibar Heroes ambazo zote
zimepangwa kundi moja katika michuano ya CECAFA Challenge mwaka huu
nchini Kenya.
Kilimanjaro
Stars imepangwa Kundi A katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika
Mashariki na Kati, CECAFA Challenge pamoja na ndugu zao, Zanzibar,
wenyeji Kenya, Rwanda na waalikwa Libya.
Katika
droo iliyopangwa jana mjini Nairobi, Kenya ambako michuano hiyo
inafanyika kuanzia Desemba 3 hadi 17, mwaka huu, Kundi B lina timu za
Uganda, Zimbabwe, Burundi, Ethiopia na Sudan Kusini.
Kilimanjaro
Stars itafungua dimba na Libya Desemba 3, mwaka huu mchezo ambao
utafuatiwa na mechi kati ya wenyeji, Kenya dhidi ya Rwanda.
Bado haifahamiki kama TFF itazuia matumizi ya jina Kilimanjaro Stars au, itarudi mezani kwa mazungumzo na wadhamini.
0 Comments