LYANGA: NINA UWEZO WA KUISAIDIA STARS , NAHESHIMU UTEUZI WA KOCHA MAYANGA

WINGA wa Fanja ya Oman, Daniel Lyanga amesema kwamba anaamini ana uwezo wa kuchezea timu ya taifa ya Tanzania, lakini anaheshimu maamuzi ya kocha wa Salum Shaaban Mayanga.
Akizungumza na JOHN NDEKI =online  kwa simu kutoka Muscat, Oman jana, Lyanga alisema kwamba anaamini wakati utafika naye ataitwa kutoa mchango wake Taifa Stars. 
“Hayo ni maamuzi ya kocha, maana yeye ndiye anachagua na anaona wapi panamfaa nani na wapi panamfaa nani. Na mimi sina tatizo na hilo, kwa kuwa wanaoitwa pia ni wachezaji kama mim na mimi itafika tu zamu yangu kama itatokea nafasi ya kuitumikia Taifa Stars nitaitwa kuitumikia,”amesema.


 Lyanga ni kiungo mshambuliaji tegemeo wa Fanja kwa sasa ambaye alijiunga na timu hiyo ya Muscat Septemba mwaka jana akitokea Simba SC ya Dar es Salaam, ambayo nayo ilimrudisha nyumbani Tanzania kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) alipokuwa akichezea Daring Club Motema Pembe (DCMP) ya Kinshasa mwaka 2015.
Tangu Septemba mwaka jana, Lyanga aliyekwenda Kongo akitokea Coastal Union ya Tanga, amecheza  mechi 26 na kufunga mabao saba, huku akiseti mabao 12 kwa krosi zake maridadi.
“Huku ninacheza sana winga zote mbili, kushoto na kulia ndiyo wananitumia sana japo msimu wa mwaka jana nilicheza namba zote za mbele hapo,”amesema.
Katika klabu hiyo, Lyanga anacheza pamoja nyota wengine wawili aliowahi kucheza nao Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, viungo Mkongo Mbuyu Twite aliyekuwa Yanga na Muivory Coast, Kipre Michael Balou aliyekuwa Azam FC, ambao wote wanaweza kucheza kama walinzi pia.
“Nipo nao wote huku na wote tunamshukuru Mungu tupo kama wachezaji muhimu kwenye timu, tunafurahia maisha,”amesema. 

Post a Comment

0 Comments