Awaua watu wa familia kwa sumu akidai wao si “wasafi” baada ya kujiunga na dhehebu.

Polisi nchini Italia wamemkamata mwanamume ambaye anadaiwa kutumia sumu ya kuua panya kuwaua watu wa familia yake kwa sababu hawakuwa “wasafi”.
Mattia Del Zotto, 27, analaumiwa kwa kuweka sumu kwenye chakula cha babu ya nyanya yake na cha shangazi ambao walifariki
Watu wengine watano katika familia wanaendelea kupata matibabu hosptalini.
Bw. Del Zotto alikamawa eneo la Mozna karibu na Milan baada polisi kupata risiti kwenye kompiuta yake.
Baada ya kukamatwa alikiri kuwa alitaka kuwaadhibu watu wasio wasafi.
Mama yake aliwaambia wachunguzi kuwa hivi karibuni alikuwa amejiunga na dhehebu.

Post a Comment

0 Comments