Miaka saba tangu Mahakama Kuu ilipomhukumu adhabu ya kunyongwa mkazi wa
Mabibo Upogoroni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, Japhary Ismail kwa
kosa la kumuua binamu yake, Mahakama ya Rufani imeibatilisha na kuamuru
kesi irudi Mahakama Kuu isikilizwe upya.
Uamuzi huo ulitolewa na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani,
lililoongozwa na Jaji Bernard Luanda, Augustine Mwarija na Rehema Mkuye
kufuatia rufaa aliyoikata mfungwa huyo kupinga hukumu aliyopewa na Jaji
Augustine Shangwa wa Mahakama Kuu.
Mahakama ya Rufani imeamuru kesi hiyo irudishwe Mahakama Kuu isikilizwe
upya baada ya kujiridhisha kuwa mwenendo wa kesi hiyo wakati wa
usikilizwaji ni batili, kutokana na makosa yaliyofanywa na washauri wa
Mahakama kwa kufanya majukumu wasiyostahili.
Kasoro hizo zilizoifanya hukumu kubatilishwa ni kitendo cha washauri hao
kumfanyia udodosaji jukumu ambalo hufanywa na wakili wa upande pinzani
katika kesi.
Kasoro hiyo iliibuliwa na Wakili aliyemwakilisha mrufani, Daniel Welwel,
katika sababu yake ya nyongeza kati ya sababu za rufaa alizokuwa
ameziwasilisha awali.
Mahakama ya Rufani katika hukumu yake iliyosomwa na naibu msajili wa
mahakama hiyo, Amir Msumi ilisema ingawa sheria haiwapi washauri wa
mahakama mwanya wa kumfanyia shahidi udodosaji, lakini katika kesi hiyo
jaji aliwapa mwanya wa kufanya hivyo kwa mashahidi wa pande zote.
Japhary alikamatwa Aprili 23, 2004 na kushtakiwa kwa tuhuma za kumuua
binamu yake, Joseph Shedula aliyekutwa amekufa chumbani walimokuwa
wamepanga huko Mabibo Upogoroni, baada ya kurejea kutoka
0 Comments