Dar es Salaam. Mtoto wa Mwanamuziki wa dansi Nguza Viking ‘Babu
Seya’ Michael Nguza amesema anamshukuru Mungu baada ya Rais John
Magufuli kutangaza familia yao ipo huru kuanzia leo Jumamosi.
Rais Magufuli ametangaza uamuzi huo, leo Jumamosi, Desemba 2017 akiwa
mjini Dodoma wakati wa akihutubia maadhimisho miaka 56 ya sherehe za
Uhuru wa Tanganyika.
Michael Nguza ambaye hivi sasa anajiita Nabii Michael baada ya kutoka
jela amesema : “Namshukuru Mungu, Mungu ni mwaminifu. Siwezi kuongea
mengi kwa sasa, nitatoa taarifa baadaye.
“Tunatarajia kufanya kikao cha familia ili kujadili suala hili na
baadaye tutaulezea umma baada ya majadiliano haya familia naomba kuweni
wavumilivu,” amesema Nabii Michael.
0 Comments